Video na Makala: Raisi Magufuli azindua Kiwanda Dar es salaam


SEKTA YA VIWANDA: KIINI CHA MAENDELEO TANZANIA
Sekta ya viwanda ina nafasi kubwa ya kukuza uchumi wa Tanzania licha ya ukweli kwamba inakabiliwa na changamoto nyingi Veneranda Sumila, Mwananchi Kwa mujibu wa aliyewahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda: sekta ya viwanda ndiyo hasa inayoshikilia ufunguo wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini kutokana na uwezo wake wa kutengeneza ajira nyingi.
Akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya sekta ya viwanda katika ukanda wa mashariki mwa Afrika, Waziri Kigoda alisema sekta hiyo siyo tu injini ya taifa katika kukuza uchumi bali pia katika kubadili maisha ya Watanzania. Ripoti hiyo ilikuwa inasisitiza kuchochea matumizi ya teknolojia, uvumbuzi, uzalishaji pamoja na kuunganisha viwanda na sekta nyingine za uchumi. Ripoti hiyo iliyozihusisha nchi za Tanzania, Burundi, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Shelisheli na Uganda, ni sehemu ya utafiti wa sekta ya viwanda uliyodhaminiwa na Kituo cha Rasilimali Ukanda wa Mashariki mwa Afrika cha Benki ya Maendeleo ya Africa. “Kunaweza kuwa na nguzo nyingine za maendeleo lakini hakuna hata moja yao inayoweza kushinda nguvu ya viwanda.
Viwanda siyo tu vinakuza uchumi kwa kuongezea bidhaa thamani bali pia vinatengeneza ajira nyingi ambazo huongeza uzalishaji,” alisema Waziri Kigoda. Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) Godfrey Simbeye aliliambia gazeti la Mwananchi katika mahojiano kwa njia ya simu kwamba nchi yoyote inayotaka kujitegemea kwenye bajeti yake, lazima kwanza iimarishwe uuzaji wa bidhaa zake zilizoongezewa thamani nje ya nchi. “Nchi inayotumia bidhaa za nje kwa wingi kama Tanzania isitarajiwe kujitegemea kibajeti. Ili nchi yoyote iepuke misaada ya kibajeti kutoka kwa wahisani, basi lazima iimarishe mauzo ya nje,” anasema Simbeye.
Faida za kuujenga uchumi wa viwanda
Uzalishaji wa bidhaa katika viwanda umekuwa msingi muhimu wa mchakato wa utandawazi ambako bidhaa nyingi zinazalishwa katika nchi fulani na kuuzwa kote duniani ilhali vipuli vya kutengenezea bidhaa hizi tena zinatoka katika nchi tofauti.
Kila nchi ina viwanda mbalimbali. Viwanda hivyo huisaidia nchi hiyo pindi iuzapo bidhaa hizo, pia huisaidia nchi husika kunufaika kiuchumi kwa uwepo wa viwanda hivyo.
Viwanda vina faida kubwa sana katika nchi yenye viwanda hivyo; faida hizo ni:
·         Kuisaidia nchi kukua kiuchumi,
·         Kupata fedha za kigeni,
·         Kulipa madeni wanayodaiwa,
·         Kuimarisha huduma za jamii,
·         Kuajiri watu ambao hawana kazi, na
·         Kunufaisha taifa kwa ujumla

HEKO RAISI WETU JPM

Comments