MAKALA: RAISI WA NIGERIA AFUATA NYAYO ZA RAISI MAGUFULI WA TANZANIA



RAISI WA NIGERIA AFUATA NYAYO ZA RAISI MAGUFULI

Katika kudhibiti matumizi mabovu ya fedha ya umma, mheshimiwa raisi Muhamad Buhari wa Nigeria kafuata nyayo za mheshimiwa raisi wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania katika kudhibiti safari za nje ya nchi zisizo na tija kwa taifa hilo kubwa barani Afrika. Hii imeonekana kuwa ni njia mojawapo ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili hela nyingi ielekezwe kwenye miradi ya maendeleo ya nchi kwa ustawi wa maisha ya wananchi wote wa jamhuri ya shirikisho ya Nigeria.

Hii inadhihirisha kuwa ili kuwa na Afrika tuitakayo kadri ya mpango wa Umoja wa Afrika (AU) uliopo sasa wa 2063, Afrika inahitaji viongozi kama raisi John Pombe Josefu Magufuli wenye uzalendo na wenye uthubutu wa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana ya mataifa yao. Ama kweli raisi Magufuli ni kioo cha bara la Afrika kwa sasa. Mungu amzidishie neema na baraka raisi Magufuli wa Tanzania.

Na Mgata Albogasto
albogasto.mgata@gmail.com

Comments