MAKALA: MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI ZA UHURU WA TANGANYIKA 2019


TANZANIA: MAADHIMISHO YA MIAKA 58 YA UHURU WA TANGANYIKA
Maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru wa Tanganyika yamefanyika leo mjini Mwanza na kuhudhuriwa na rais John Pombe Magufuli. Kwa mara ya kwanza chama cha upinzani Chadema pia kimeshiriki kwenye maadhimisho hayo.
    
Tansania Feier 58 Jahre Unabhängigkeit (DW/D. Bulendu)
Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema kwa mara ya kwanza leo kinashiriki sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika ikiwa ni hatua ya aina yake. Chama hicho kimekuwa kikisusia sherehe hizo tangu mwaka 2015 ulipofanyika uchaguzi mkuu kama ishara ya kupinga matokeo ya urais wa wakati huo. 

Kushiriki kwa Chadema kwenye sherehe hizi kunatuma ujumbe mpya kuhusu siasa za Tanzania hasa wakati ambapo hamasa ya kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020 ikiwa ni mada inayojadiliwa na kila chama.

Chadema ambayo imekuwa ikisizusia sherehe hizi inajumuika na viongozi wa serikali na wale wa chama tawala cha CCM katika wakati ambapo vigogo wakuu waliojiunga na chama hicho wakati wa vuguvugu la uchaguzi uliopita wakiwa wamejiondoa ndani ya chama hicho wengine wakirejea kwenye chama chao kilichowakuza CCM.

Ingawa hatua hii ya Chadema kushiriki kwa mara ya kwanza tangu ulipomalizika uchaguzi uliopita, imewavutia wengi wakidadisi sababu zilizopo nyuma ya pazia, hata hivyo baadhi ya wachambuzi wa mambo wanasema kuwa huenda chama hiki kinaanza kuweka mguu sawa kuelekea uchaguzi ujao.

Baadhi ya watumbuizaji wakati wa maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru wa Tanganyika
Baadhi ya watumbuizaji wakati wa maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru wa Tanganyika

Hoja hiyo inapata mashiko na kauli ya chama hicho kinachosema kwamba hakioni sababu ya kuendelea kujiweka kando na sherehe hizo kwa vile kinajiandaa kushika dola katika uchaguzi ujao. Mkurugenzi wa itifaki na mambo ya nje ya chama hicho, John Mrema, amesema suala la chama hicho kuamua kushiriki sherehe za mwaka huu ni tafsiri inayoakisi mwelekeo mpya wa chama hicho kuelekea siasa za usoni.

Wakati Chadema kikijumuika na viongozi wengine wa chama na chama tawala, CCM kwenye maadhimisho hayo, chama kingine cha upinzani ACT-Walendo kimesusia sherehe hizo kwa madai kuwa hakioni sababu ya kushiriki wakati hakuna uhuru wa maoni, demokrasia kuzidi kubanwa na vyama vya upinzani kuendelea kuandamwa na dola.

Afisa habari wa chama hicho, Suphiani Juma amesema hizo ni baadhi ya sababu za msingi zinazokifanya chana hicho kususia sherehe hizo.

Katika sherehe hizi, Chadema imeongozwa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe aliyeambatana na wabunge kadhaa. 

_________________________________
Siasa na Ukoloni

Karne kadhaa kabla ya mwaka huu, Tanganyika ilikuwa koloni ya Urenu kuanzia karne ya 15 had ya 17, ambapo Sultan wa Oman akashika nchi. Baada ya hapo, Ujerumani iliongeza Tanganyika katika orodha yake ya wakoloni mpaka Vita Kuu 1. Baada ya hapo, Uingereza uliiweka chini ya uongozi wa Shirikisho la Mataifa. Hata hivyo, Taganyika ilipata uhuru wake Desemba 9 mwaka 1961 kutoka kwa ukoloni wa Waingereza. Ila, chakushangaza kidogo ni kwamba siku hii ndio iliyokubalika kama siku ya uhuru ya Tanzania, wakati Tanzania haikuwepo had Aprili 26th 1964.
Ingawa matukio haya ni muhimu katika historia ya Tanzania, kuna mengine kama:
1967 – Kwenye Maadhimisha ya Arusha, Nyerere alianzisha rasmi mchakato wa ujamaa na uchumi wa kujitegemea
1977 – Chama Cha Mapinduzi linaundwa baada ya TANU na ASP kuungana.
1978 – Majeshi ya Uganda yanaingia na kutawala kipande cha nchi.
1979 – Majeshi ya Tanzania yanaingia Uganda, yakikamata Kampala, mji mkuu, na kusaidia kumtoa Rais Idi amin
1985 – Nyere anastaafu na Rais wa Zanzibar, Ali Hassan Mwinyi, anakuwa Rais wa Tanzania.
1992 – Katiba inarekebishwa kuruhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa
1995 – Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi unafanyika
Historia ya Kiasili na Utamaduni
Olduvai Gorge
Kuna uhusiano gani kati ya mkonge na Olduvai Gorge? Zote zipo kwenye maeneo ambapo ushaidi wa mababu wa kwanza kwa binadamu, upo. Jina la Olduvai Gorge, ambayo ni ukosefu wa kuandika Oldupai ambayo ni jina la mimea ya mkonge yanayoota hapo, uligunduliwa na Loui na Mary Leakey kati ya miaka ya 1930 – 1950. Sasa, hii inamaanisha kwamba mababu ya binadamu walikuwa watanzania? Huwezi jua!
Makabila  
Tanzania ina zaidi ya makabila 120 na ilipata uhuru bila damu kumwagika.
Kati ya makabila haya, 4 zinajulikana zaidi ya zingine kwa zababu tofauti, zikiwemo:
·         Wasukuma, kabila kubwa zaidi Tanzania
·         Wachagga, kabila inayojulikana kwa kufanya biashara
·         Wamakonde, kabila inayojulikana kwa vinyago vya mbao
·         Wamasai, wapiganaji hodari na wafugaji.
Lugha
Kiswahili ni mchanganyiko wa lahaja za kibantu pamoja na kiarabu. Nyerere alikuwa mpiga debe mkubwa wa Swahili na ikawa lugha ya taifa ya Tanzania. Hii imesaidia kuweka umoja kwenye nchi ilio na zaidi ya kabila 120, zote zikiwa na lugha yao.
Salamu na kusalimiana ni kitu muhimu kwenye utamaduni wa Tanzania. Iwe unaingia ofisini, umeenda dukani au unakutana na marafiki, kusalimiana na ulionao au walio karibu nawe ni muhimu. Pia, ‘Jambo’ sio salamu inayotumika Tanzania. Salamu ya kawaida ni Habari/Habari yako/Habari za saa hizi. Salamu zisizo rasmi ni kama Mambo/Mambo vipi?/kwema?/ Salama?
Nguo na Vitambaa Asili
Tanzania ina aina mbili za mavazi zinazojulikana kokote nchini.
Kanga ni kitambaa cha pamba linalo valiwa na wanawake, iki fungwa kiunoni kwenda chini. Asili yake ni ni kutoka wanawake wa Zanzibar katika karne ya 19. Ni nyepesi, yenye rangirangi na inamatumizi mengi kama taulo, scafu ya kichwani na mengineyo. Umaarufu wake umekuwa na siku hizi ni kawaida kukuta methali ikiwa imeandikwa kwenye kanga.
Kitenge,ina rangi kali na nzitu zinazoendana na michoro yaliyomo. Tofauti kubwa kati ya kitenge na n kanga ni kwamba kitenge ni nzito zaidi. Pia, siku hizi bukta, mashati na t-shirt za kitenge zimeenea mjini. Zaidi ya hapo, mitindo ya vitenge vimeanze kuonekana kwenye dunia ya mitindo na mavazi.
Jiografia
Tanzania inajisifia sana kwa kuwa ina Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kuliko zote Africa na Ziwa Viktoria, ziwa inyokwenda chini kuliko yote. Kuelewa ukubwa wa Tanzania vizuri, iko mpakani na Kenya na Uganda (Kaskazini); Burundi, Rwanda na DRC (Magharibi) na Msumbiji, Zambia na Malawi (Kusini). Ongezea bahari la India lilo pwani, na utaanza kuelewa ukubwa wa Tanzania.
Ukipata muda, funga safari za kwenda Kilimanjaro kutoka Dar es Salaam ukisindikizwa na milima ya Usambara, kwa mfano. Kun mengi ya kuona!
Nchi ya Amani
Kuanzia siasa na watu wake, ardhi na lugha, historia ya Tanzania ina mambo mengi. Kwa ujumla, watanzania ni watu tulivu wenye heshima na uvumulivu. Nchi hii imetoka mbali na inajiendeleza polepole ila vizuri. Ila kuna matatizo makubwa mbali mbali. Lakini, kwa kifupui nchi inaendelea vizuri.
___________________________________________
The History of Tanzania started with the European Colonialists.  The 8th century saw the growth of city states along the coast after settlement by Arabs as a nation from Oman. It was seven centuries later in 1499 that the Portuguese navigator Vasco da Gama visited the island of Zanzibar.  Another 100 years later in the 16th century, the Portuguese occupied Zanzibar. Their occupation did not last for long as in 1699 the Portuguese were ousted from Zanzibar by Arabs of Oman who had returned to make it their own.  So in the 18th century the Sultan of Oman reasserted Arab overlord ship of the East African coast, which became subordinate to Zanzibar.

By 1840 when Sultan Seyyid bin Sultan moved his capital from Oman to Zanzibar, trade in slaves and ivory flourished.  In 1861, the Sultanates of Zanzibar and Oman separated on the death of Seyyid. During the 19th century, Europeans started to explore inland, closely followed by Christian missionaries. In 1884 the German Colonization Society began to acquire territory on the mainland in defiance of Zanzibar and 1890 Britain obtained protectorate status over Zanzibar, abolished the slave trade, and recognised German claims to the Mainland. German East Africa was formally established as a colony in 1897.

The 1905-07 Majimaji revolt was brutally suppressed by German troops. World events then took over with the outbreak of the First World War, and far as it was from Europe, German East Africa was not immune from the fighting, though effective fighting was short lived due to the successful 1916 Conquest of German East Africa by the British. In 1919, the League of Nations gave Britain a mandate to administer part of German East Africa, known as Tanganyika. In 1946 Tanganyika became a UN trust territory.

A Legislative Council was set up in 1926; it was enlarged in 1945 and restructured in 1955 to give equal representation to Africans, Asians and Europeans, sitting as 30 "'un-officials" with the 31 "officials". In 1954, a schoolteacher, Julius Nyerere, founded the Tanganyika African National Union (TANU), which promoted African nationalism and won a large public following campaigning for independence. The colonial authorities responded with constitutional changes increasing the voice of the African population while reserving seats for minority communities.

Elections were held in 1958 and again in 1960. The result was an overwhelming victory for TANU, which was by this time campaigning for independence as well as majority rule. The new government and British Government agreed at a constitutional conference in London to full independence for Tanganyika in December 1961. Zanzibar achieved independence in 1963 as a separate and sovereign country, under the al-Busaidy Sultan.

Tanganyika became a republic in December 1962, one year after achieving independence, and the direct presidential election brought TANU’s leader, Julius Nyerere, to the presidency. In 1965 the Constitution was changed to establish a one-party system. Meanwhile, in Zanzibar, a revolution had overthrown the Arab Sultan on 12th January 1964. One month after independence the Constitution was abrogated; Abedi Amani Karume was declared the first African President of Peoples’ Republic of Zanzibar and the country became a one-party state under the Afro-Shirazi Party.

On 26th April 1964 Tanganyika and Zanzibar united as the United Republic of Tanzania, with Julius Nyerere as President and the head of state, while Karume as his Vice President, retained at the same time the Presidency of Zanzibar. In 1971 Karume was assassinated in Zanzibar and Aboud Jumbe succeeded him as President of Zanzibar and Vice President of Tanzania. The political union between Zanzibar and mainland Tanzania has weathered more than four decades of change. Zanzibar has its own parliament and president.

In an effort to create socially equitable and rapid development, it became in early proponent of African socialism, Ujamaa (roughly meaning Togetherness), launched in 1967 under the banner of Arusha Declaration, with nationalisation of banking, finance, industry and large-scale trade, marketing through boards, and the resettlement of peasants in communal villages, Vijiji vya Ujamaa , created out of large estates.

In 1977, the two ruling parties: TANU and Afro Shirazi Party, merged to form the Chama Cha Mapinduzi (CCM) which continues to rule the country after consecutive successful elections.
___________________________________________

Comments